TOTTENHAM YAMGEUKIA CHRIS SMALLING, NI BAADA YA UJO WA BEKI MPYA NDANI YA MAN UNITED - JONGOTZMEDIA.COM

Latest

efm

">">WHATSAPP NUMBER 0757357341

Pages

Monday, 19 June 2017

TOTTENHAM YAMGEUKIA CHRIS SMALLING, NI BAADA YA UJO WA BEKI MPYA NDANI YA MAN UNITED

   Kocha wa  Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino anaweza kumgeukia beki wa Manchester United, Chris Smalling baada ya kukwama kumsajili beki wa Leicester City, Harry Maguire.
Pochettino anahitaji beki wa kati ili kuongeza ushindani kwa Toby Aiderweireld na Jan Vertonghen bada ya timu hiyo kuwa na msimu mzuri kiasi cha kushika nafasi ya pili katika Premier League msimu uliopita.

Smalling yupo shakani kukosa namba kwenye kikosi chake kutokana na ushindani utakaokuwepo hasa kutokana na ujio wa Victor Lindelof aliyesajiliwa kwa pauni milioni 31.

Smalling amekuwa akipata wakati mgumu kupata nafasi chini ya Kocha Jose Mourinho ambaye amekuwa aonyeshi kumuamini moja kwa moja mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment